يُوسُفُ أَعۡرِضۡ عَنۡ هَٰذَاۚ وَٱسۡتَغۡفِرِي لِذَنۢبِكِۖ إِنَّكِ كُنتِ مِنَ ٱلۡخَاطِـِٔينَ
Yusuf! Wachilia mbali haya. Na wewe, mwanamke, omba msamaha kwa dhambi zako. Kwa hakika wewe ni katika walio fanya makosa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Akasema kiongozi wa Misri, «Ewe Yūsuf! acha kutaja mambo yaliykuwa kutoka kwake na usimwambie yoyote. Na uombe msamaha wa dhambi zako kwa Mola wako, ewe mwanamke, iwapo wewe ni miongoni mwa wale waliofanya hatia kwa kumtaka Yūsuf kimapenzi bila ya yeye kutaka na kwa kumzulia urongo.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس