وَقَالَ ٱلَّذِي نَجَا مِنۡهُمَا وَٱدَّكَرَ بَعۡدَ أُمَّةٍ أَنَا۠ أُنَبِّئُكُم بِتَأۡوِيلِهِۦ فَأَرۡسِلُونِ
Hapo akasema yule aliye okoka katika wale wawili akakumbuka baada ya muda: Mimi nitakwambieni tafsiri yake. Basi nitumeni.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hapo akasema yule aliyeokoka na kuuawa kati ya marafiki wawili wa Yūsuf ndani ya jela, na akakumbuka habari ya Yūsuf baada ya muda kupita, «Mimi nitawapa habari ya tafsiri ya ndoto hii. Nitumeni kwa Yūsuf nipate kuwaletea uaguzi wake.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس