وَلَمَّا دَخَلُواْ مِنۡ حَيۡثُ أَمَرَهُمۡ أَبُوهُم مَّا كَانَ يُغۡنِي عَنۡهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن شَيۡءٍ إِلَّا حَاجَةٗ فِي نَفۡسِ يَعۡقُوبَ قَضَىٰهَاۚ وَإِنَّهُۥ لَذُو عِلۡمٖ لِّمَا عَلَّمۡنَٰهُ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَعۡلَمُونَ
Na walipo ingia kama alivyo waamrisha baba yao, haikuwafaa kitu kwa Mwenyezi Mungu, isipo kuwa ni haja tu iliyo kuwa katika nafsi ya Yaa'qub aliitimiza. Na hakika yeye alikuwa na ilimu kwa sababu tulimfundisha; lakini watu wengi hawajui.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na walipoingia kupitia milango mbalimbali, kama alivyowaamrisha baba yao, hilo halikuwa ni lenye kuwazuilia uamuzi wa Mwenyezi Mungu kwao, isipokuwa ilikuwa ni huruma ndani ya moya wa Ya’qūb juu yao wasipatikane na jicho la husuda. Na Ya’qūb ni mwenye ujuzi mkubwa wa mambo ya Dini yake aliyofundishwa na Mwenyezi Mungu kwa njia ya wahyi, lakini wengi wa watu hawajui mwisho wa mambo na undani wake, na pia hawayajui anayoyajua Ya’qūb, amani imshukie, katika mambo ya Dini yake..
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس