وَلَمَّا دَخَلُواْ عَلَىٰ يُوسُفَ ءَاوَىٰٓ إِلَيۡهِ أَخَاهُۖ قَالَ إِنِّيٓ أَنَا۠ أَخُوكَ فَلَا تَبۡتَئِسۡ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Na walipo ingia kwa Yusuf alimchukua nduguye akasema: Mimi hakika ni nduguyo. Basi usihuzunike kwa waliyo kuwa wakiyafanya.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na walipoingia ndugu zake Yūsuf kwake, katika nyumba yake ya kukaribisha wageni, wakiwa pamoja na ndugu yake wa kwa baba na mama, Yusuif alimkumbatia nduguye wa kwa baba na mama na akamwambia kwa siri, «Mimi ni ndugu yako. Basi usihuzunike wala usiingiwe na dhiki kwa yale waliyonifanyia kipindi kilichopita.» Na akamuamuru alifiche jambo hilo kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس