Al-Kahf
ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ عَلَىٰ عَبۡدِهِ ٱلۡكِتَٰبَ وَلَمۡ يَجۡعَل لَّهُۥ عِوَجَاۜ
Kuhimidiwa ni kwa Mwenyezi Mungu, ambaye amemteremshia mja wake Kitabu, wala hakukifanya kina upogo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, kwa kuwa Ana sifa ambazo zote ni sifa za ukamilifu na kwa kuwa ana neema zilizo wazi na zilizofichika, za kidini na za kidunia, Ambaye Alifanya wema Akamteremshia mja Wake na Mtume Wake Muhammad, rehema za Mwenyezi Mungu na amani zimshukiye, Qur’ani na Asiifanye iwe na kitu chochote cha kupotoka na haki.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس