وَأَذِّن فِي ٱلنَّاسِ بِٱلۡحَجِّ يَأۡتُوكَ رِجَالٗا وَعَلَىٰ كُلِّ ضَامِرٖ يَأۡتِينَ مِن كُلِّ فَجٍّ عَمِيقٖ
Na watangazie watu Hija; watakujia kwa miguu na juu ya kila ngamia aliye konda, wakija kutoka katika kila njia ya mbali.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
na uwajulishe watu, ewe Ibrāhīm, uwajibu wa Hija juu yao, watakujia kwa kila namna zao, wakiwa wanatembea kwa miguu na wakiwa wanapanda, miongoni mwa ngamia, kila aliyeambata matumbo kwa kutembea na kufanya kazi na sio kwa udhaifu. Watakuja kutoka njia ya mbali,
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس