وَلِكُلِّ أُمَّةٖ جَعَلۡنَا مَنسَكٗا لِّيَذۡكُرُواْ ٱسۡمَ ٱللَّهِ عَلَىٰ مَا رَزَقَهُم مِّنۢ بَهِيمَةِ ٱلۡأَنۡعَٰمِۗ فَإِلَٰهُكُمۡ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ فَلَهُۥٓ أَسۡلِمُواْۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُخۡبِتِينَ
Na kila umma tumewafanyia mahala pa kuchinjia mihanga ya ibada ili walitaje jina la Mwenyezi Mungu juu ya vile walivyo ruzukiwa katika wanyama wa mifugo. Basi Mungu wenu ni Mungu Mmoja tu. Jisalimishieni kwake tu, na wabashirie wanyenyekevu,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kila kundi lenye kuamini lililotangulia, tumelifanyia mambo ya ibada ya kuchinja na kumwaga damu, hayo ni kwa ajili wapate kutaja jina la Mwenyezi Mungu Aliyetukuka wakati wa kuchinja kile tulichowaruzuku cha hawa wanyama-howa na wamshukuru. Basi Mola wenu, enyi watu, ni Mola Mmoja, Yeye ni Mwemyezi Mungu. Hivyo basi iandameni amri Yake na amri ya Mtume Wake. Na uuwape bishara njema, ewe Mtume, wale wanyenyekevu waliosalimu amri kwa Mola wao, kwamba watapata kheri mbili: ya ulimenguni nay a Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس