وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يُجَٰدِلُ فِي ٱللَّهِ بِغَيۡرِ عِلۡمٖ وَلَا هُدٗى وَلَا كِتَٰبٖ مُّنِيرٖ
Na katika watu wapo wanao bishana juu ya Mwenyezi Mungu bila ya ilimu, wala uwongofu, wala Kitabu chenye nuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Miongoni mwa makafiri kuna wenye kujadili kwa njia ya ubatilifu kuhusu Mwenyezi Mungu na kuhusu kumpwekesha Yeye na kuhusu kumteua Kwake Mitume wake, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, na kuhusu kuteremsha Kwake Qur’ani. Kujadili huko ni bila ya ujuzi, ufafanuzi wala kitabu kitokacho kwa Mwenyezi Mungu chenye ushahidi na hoja iliyo wazi,
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس