وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَيَعۡلَمَنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ
Na hapana shaka Mwenyezi Mungu atawatambulisha walio amini, na atawatambulisha wanaafiki.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Atawajua Mwenyezi Mungu, tena atawajua, ujuzi wenye kujitokeza kwa viumbe, wale waliomuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakazifuata Sheria Zake kivitendo, na Atawajua, tena Atawajua, wanafiki, ili Alipambanue kila kundi na lingine.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس