وَتِلۡكَ ٱلۡأَمۡثَٰلُ نَضۡرِبُهَا لِلنَّاسِۖ وَمَا يَعۡقِلُهَآ إِلَّا ٱلۡعَٰلِمُونَ
Na hiyo ni mifano tunawapigia watu, na hawaifahamu ila wenye ilimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na mifano hii tunawapigia watu , ili wanufaike nayo na wajifunze kwayo. Na hawaielewi isipokuwa wale wanaomjua Mwenyezi Mungu na kuzijua aya Zake na Sheria Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس