وَلَمۡ يَكُن لَّهُم مِّن شُرَكَآئِهِمۡ شُفَعَـٰٓؤُاْ وَكَانُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ كَٰفِرِينَ
Wala hawatakuwa na waombezi miongoni mwa walio kuwa wakiwashirikisha na Mungu; na wao wenyewe watawakataa hao washirikishwa wao.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na washirikina , Siku hiyo, hawatokuwa na waombezi kati ya waungu wao waliokuwa wakiwaabudu badala ya Mwenyezi Mungu, bali wao, hao waungu, watajiepusha nao na wao watajiepusha nao. Maombezi ni ya Mwenyezi Mungu Peke Yake, na hayatafutwi kutoka kwa mwingine.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس