وَدُّواْ لَوۡ تَكۡفُرُونَ كَمَا كَفَرُواْ فَتَكُونُونَ سَوَآءٗۖ فَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ أَوۡلِيَآءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ وَجَدتُّمُوهُمۡۖ وَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرًا
Wanapenda lau kuwa nanyi mnge kufuru kama walivyo kufuru wao, ili muwe sawa sawa. Basi msiwafanye marafiki miongoni mwao mpaka wahame kwa ajili ya Dini ya Mwenyezi Mungu. Na wakikengeuka basi wakamateni na wauweni popote mnapo wapata. Wala msimfanye rafiki katika wao wala msaidizi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hawa wanafiki waliwatamania nyinyi Waumini lau mlikanusha uhakika wa lile ambalo nyoyo zenu zimeliamini kama vile wao walivyolikanusha kwa nyoyo zao, ili muwe sawa na wao katika kukanusha. Basi msiwafanye ni wasafiwa wenu mpaka wagure katika njia ya Mwenyezi Mungu kama ushahidi wa ukweli wa Imani yao. Basi wakiyakataa yale waliyolinganiwa kwayo, washikeni popote waliopo na muwaue, wala msimfanye yoyote katika wao kuwa ni msimamizi badala ya Mwenyezi Mungu wala ni mwokozi ambaye mnataka awaokoe.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس