ثُمَّ لَمۡ تَكُن فِتۡنَتُهُمۡ إِلَّآ أَن قَالُواْ وَٱللَّهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشۡرِكِينَ
Kisha hautakuwa udhuru wao ila ni kusema: Wallahi! Mola wetu Mlezi! Hatukuwa washirikina.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha hayakuwa majibu yao, walipojaribiwa na kupewa mtihani kwa kuulizwa kuhusu washirika wao, isipokuwa walijitoa na wao na wakaapa kwamba wao hawakuwa ni wenye kumshirikisha yoyote na Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس