وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَمَسُّهُمُ ٱلۡعَذَابُ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ
Na walio kanusha Ishara zetu itawagusa adhabu kwa walivyo kuwa wakipotoka.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wale waliozikanusha aya zetu za Qur’ani na miujiza, hao itawapata adhabu Siku ya Kiyama kwa sababu ya ukafiri wao na kutoka kwao kwenye twaa ya Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس