دَعۡوَىٰهُمۡ فِيهَا سُبۡحَٰنَكَ ٱللَّهُمَّ وَتَحِيَّتُهُمۡ فِيهَا سَلَٰمٞۚ وَءَاخِرُ دَعۡوَىٰهُمۡ أَنِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Wito wao humo utakuwa: Subhanaka Llahumma "Umetakasika Ee Mwenyezi Mungu!" Na maamkio yao humo ni "Salama". Na mwisho wa wito wao ni: Alhamdulillahi Rabbil A'lamiin "Kuhimidiwa kote ni kwa Mwenyezi Mungu, Mola Mlezi wa walimwengu wote."
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Maombi yao Peponi ni kuleta tasbihi (kusema Subhānaka Allāhumma), na maamkizi ya Mwenyezi Mungu na Malaika Wake kuwaamkia wao, na maamkizi yao, wao kwa wao, huko Peponi ni Salām. Na mwisho wa maombi yao ni kusema kwao, «Al-hamdu li Llāhi Rabbil- 'ālamīn» Yaani, shukrani na sifa njema ni za Mwenyezi Mungu, Muumba viumbe na Mwenye kuvilea kwa neema Zake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس