إِنَّ ٱلَّذِينَ حَقَّتۡ عَلَيۡهِمۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ لَا يُؤۡمِنُونَ
Hakika wale ambao neno la Mola wako Mlezi limekwisha thibitika juu yao, hawataamini,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika ya wale ambao limethibiti kwao neno la Mola Wako la kuwafukuza kwenye rehema Yake na kuwaadhibu, hawaziamini hoja za Mwenyezi Mungu, hawaukubali upweke Wake wala hawazifuati sheria Zake kivitendo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس