أَرۡسِلۡهُ مَعَنَا غَدٗا يَرۡتَعۡ وَيَلۡعَبۡ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ
Mpeleke kesho pamoja nasi, ale kwa furaha na acheze; na bila ya shaka sisi tutamhifadhi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Tuachie awe na sisi kesho tutakapotoka kwenda kwenye malisho ya wanyama wetu, apate kutembea, apumbae, afurahike na acheze kwa kushindana na mfano wake miongoni mwa machezo yanayofaa. Na sisi ni wenye kumtunza na kila unalomuogopea.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس