وَٱتَّبَعۡتُ مِلَّةَ ءَابَآءِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ مَا كَانَ لَنَآ أَن نُّشۡرِكَ بِٱللَّهِ مِن شَيۡءٖۚ ذَٰلِكَ مِن فَضۡلِ ٱللَّهِ عَلَيۡنَا وَعَلَى ٱلنَّاسِ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يَشۡكُرُونَ
Na nimefuata mila ya baba zangu, Ibrahim, na Is-haq, na Yaa'qub. Hatuna haki ya kumshirikisha Mwenyezi Mungu na chochote. Hiyo ni katika fadhila ya Mwenyezi Mungu juu yetu na juu ya watu; lakini watu wengi hawashukuru.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na nimefuata Dini ya baba zangu: Ibrāhīm, Is’ḥāq na Ya’qūb, ndipo nikaamuabudu Mwenyezi Mungu Peke Yake. Haikuwa kwetu sisi kumfanyia Mwenyezi Mungu mshirika katika kumuabudu. Kumpwekesha Mwenyezi Mungu huko, kwa kumhusu Yeye Peke Yake kwa ibada, ni miongoni mwa yale ambayo Mwenyezi Mungu Ametutunukia sisi na watu, lakini wengi zaidi wa watu hawamshukuru Mwenyezi Mungu kwa neema ya upwekeshaji wa Mwenyezi Mungu na Imani.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس