يُوسُفُ أَيُّهَا ٱلصِّدِّيقُ أَفۡتِنَا فِي سَبۡعِ بَقَرَٰتٖ سِمَانٖ يَأۡكُلُهُنَّ سَبۡعٌ عِجَافٞ وَسَبۡعِ سُنۢبُلَٰتٍ خُضۡرٖ وَأُخَرَ يَابِسَٰتٖ لَّعَلِّيٓ أَرۡجِعُ إِلَى ٱلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Yusuf! Ewe mkweli! Tueleze nini maana ya ng'ombe saba wanene kuliwa na ng'ombe saba walio konda. Na mashuke saba mabichi na mengine makavu, ili nirejee kwa watu wapate kujua.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Alipofika yule mtu kwa Yūsuf alimwambia, «Yūsuf! Ewe mkweli sana! Tuagulie ndoto ya aliyeota ng’ombe saba wanono wanaliwa na ng’ombe saba waliokonda, na akaona masuke saba mabichi na mengine makavu. Natarajia nitarudi kwa mfalme na marafiki zake niwape tafsiri ya hiyo niliyokuuliza na ili wapate kujua cheo chako na utukufu wako.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس