قَالَ هَلۡ ءَامَنُكُمۡ عَلَيۡهِ إِلَّا كَمَآ أَمِنتُكُمۡ عَلَىٰٓ أَخِيهِ مِن قَبۡلُ فَٱللَّهُ خَيۡرٌ حَٰفِظٗاۖ وَهُوَ أَرۡحَمُ ٱلرَّـٰحِمِينَ
Je, nikuaminini kwa huyu ila kama nilivyo kuaminini kwa nduguye zamani? Lakini Mwenyezi Mungu ndiye Mbora wa kulinda, naye ndiye Mbora wa kurehemu kuliko wenye kurehemu wote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Baba yao akawaambia, «Vipi nitawaamini juu ya Binyāmīn, na nilishawaamini juu ya Yūsuf kabla yake, mkaahidi kumhifadhi na msilitekeleze hilo? Mimi siziamini ahadi zenu na utunzi wenu, lakini mimi nauamini utunzi wa Mwenyezi Mungu, Bora wa wenye kutunza na Mwenye huruma zaidi kuliko wenye huruma. Namtarajia Anirehemu, Amtunze na Amrudishe kwangu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس