قَالَ إِنَّمَآ أَشۡكُواْ بَثِّي وَحُزۡنِيٓ إِلَى ٱللَّهِ وَأَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Akasema: Hakika mimi namshitakia Mwenyezi Mungu sikitiko langu na huzuni yangu. Na ninajua kwa Mwenyezi Mungu msiyo yajua nyinyi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ya’qūb akasema kuwajibu, «Simuonyeshi hamu yangu na masikitiko yangu isipokuwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Yeye Ndiye Mwenye kuondoa shida na matatizo. Na ninayajua, kuhusu rehema ya Mwenyezi Mungu na maliwazo Yake, mambo msiyoyajua.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس