يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ
Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao. Na kwa Mwenyezi Mungu yatarejeshwa mambo yote.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Anayajua yaliyo mbele ya Malaika wake na Mitume Wake kabla hajawaumba, na Anayajua yenye kuwa baada ya kutoweka kwao. Na kwa Mwenyezi Mungu, Peke Yake, yanarejea mambo yote.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس