ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَلَىٰ رَبِّهِمۡ يَتَوَكَّلُونَ
Ambao walisubiri, na wakamtegemea Mola wao Mlezi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mabustani hayo yaliyotajwa ni ya Waumini waliovumilia katika kumuabudu Mwenyezi Mungu, wakashikamana na dini yao na wakawa wanamtegemea Mwenyezi Mungu katika riziki zao na kupigana jihadi na maadui wao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس