سَتَجِدُونَ ءَاخَرِينَ يُرِيدُونَ أَن يَأۡمَنُوكُمۡ وَيَأۡمَنُواْ قَوۡمَهُمۡ كُلَّ مَا رُدُّوٓاْ إِلَى ٱلۡفِتۡنَةِ أُرۡكِسُواْ فِيهَاۚ فَإِن لَّمۡ يَعۡتَزِلُوكُمۡ وَيُلۡقُوٓاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ وَيَكُفُّوٓاْ أَيۡدِيَهُمۡ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ ثَقِفۡتُمُوهُمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكُمۡ جَعَلۡنَا لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينٗا
Mtawakuta wengine wanataka wapate salama kwenu na salama kwa watu wao. Kila wakirudishwa kwenye fitna hudidimizwa humo. Ikiwa hawajitengi nanyi, na wakakuleteeni salama, na wakazuia mikono yao, basi wakamateni na wauweni popote mnapo wakuta. Na juu ya hao ndio tumekupeni hoja zilizo wazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mtawapata watu wengine miongoni mwa wanafiki wanapenda kuzituliza nafsi zao upande wenu kwa kuwaonyesha kuwa wana Imani na pia wanapenda kujituliza upande wa watu wao walio makafiri kwa kuwaonyesha kuwa wao wako kwenye ukafiri. Kila wakirudishwa kwenye mahali pa ukafiri na makafiri, huingia kwenye hali mbaya zaidi. Basi hawa wasipojiepusha na nyinyi, wakajisalimisha kwenu kikamilifu na wakajizuia wasipigane na nyinyi, washikeni kwa nguvu na muwaue popote waliopo. Wale ndio ambao waliofikia, katika njia hii mbaya sana, kiasi cha kuwapambanua wao na wasiokuwa wao; wao ndio ambao tumewapa nyinyi hoja iliyo wazi ya kuwaua na kuwateka.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس