وَمَا يُؤۡمِنُ أَكۡثَرُهُم بِٱللَّهِ إِلَّا وَهُم مُّشۡرِكُونَ
Na wengi katika wao hawamuamini Mwenyezi Mungu pasina kuwa ni washirikina.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na hawa wenye kuzipa mgongo dalili za Mwenyezi Mungu hawakubali kwamba Mwenyezi Mungu ni Mwenye kuwaumba, ni Mwenye kuwapa riziki, ni Muumba wa kila kitu na ni Mstahiki wa kuabudiwa isipokuwa katika hali ya kumshirikisha kwa kuabudu kwao masanamu na mizimu. Mwenyezi Mungu Ametukuka na kuepukana na hilo kabisa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس