ثُمَّ بَدَا لَهُم مِّنۢ بَعۡدِ مَا رَأَوُاْ ٱلۡأٓيَٰتِ لَيَسۡجُنُنَّهُۥ حَتَّىٰ حِينٖ
Basi ikawadhihirikia baada ya kuona Ishara kuwa wamfunge kwa muda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Kisha ikamdhihirikia waziri na marafiki zake, baada ya kuziona dalili za kuwa Yūsuf hana hatia na amejiepusha na machafu, wamfunge mpaka muda fulani, mrefu au mfupi, ili kuzuia fedheha.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس