ذَٰلِكَ لِيَعۡلَمَ أَنِّي لَمۡ أَخُنۡهُ بِٱلۡغَيۡبِ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي كَيۡدَ ٱلۡخَآئِنِينَ
Hayo ni apate kujua ya kwamba mimi sikumfanyia khiyana nyuma yake; na ya kwamba Mwenyezi Mungu haziongoi hila za makhaini.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Neno hilo nililolisema la kumwepushia Yūsuf tuhuma na kuikubalia makosa mimi mwenyewe ni kwa ajili mume wangu ajue kwamba mimi sikumfanyia hiana kwa kumzulia urongo na hayakutukia machafu kutoka kwangu pamoja na kuwa nilimtaka Yūsuf. Nimekubali hilo ili kuonyesha wazi kuwa mimi sina hatia wala yeye hana hatia na kwamba Mwenyezi Mungu Hawaafikii wala Hawaongozi wenye kufanya hiana katika uhaini wao.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس