فَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَرِزۡقٞ كَرِيمٞ
Basi walio amini na wakatenda mema watapata maghfira na riziki za ukarimu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Basi wale wenye kumuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, na imani hiyo ikajikita kwenye nyoyo zao na wakafanya matendo mema, watapata msamaha wa dhambi zao kutoka kwa Mola wao na sitara ya kufinika matendo ya uasi yaliyotokana na wao na riziki nzuri isiyokatika nayo ni Pepo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس