وَإِن جَٰدَلُوكَ فَقُلِ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ
Na wakikujadili basi sema: Mwenyezi Mungu anajua zaidi mnayo yatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wakishikilia kujadiliana na wewe kwa njia ya ubatilifu kuhusu yale unayowalingania nayo, usijadiliane na wao, bali waambie, «Mwenyezi Mungu ni mjuzi zaidi wa mnayoyafanya ya ukafiri na kukanusha,» kwani wao wanafanya inadi na kiburi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس