تَبَارَكَ ٱلَّذِيٓ إِن شَآءَ جَعَلَ لَكَ خَيۡرٗا مِّن ذَٰلِكَ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ وَيَجۡعَل لَّكَ قُصُورَۢا
Ametukuka ambaye akitaka atakujaalia yaliyo bora kuliko hayo, nayo ni mabustani yapitayo mito kati yao, na atakujaalia majumba ya fakhari.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni kubwa mno baraka za Mwenyezi Mungu, na ni mengi sana mema Yake, Ambaye Akitaka Atakufanyia mema zaidi kuliko yale waliotamani uwe nayo, Angalikufanyia, ulimwenguni, mashamba mengi ambayo kati yake inapita mito, na Akufanye uwe na majumba makubwa ya fahari.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس