قُلۡ مَا يَعۡبَؤُاْ بِكُمۡ رَبِّي لَوۡلَا دُعَآؤُكُمۡۖ فَقَدۡ كَذَّبۡتُمۡ فَسَوۡفَ يَكُونُ لِزَامَۢا
Sema: Mola wangu Mlezi asinge kujalini lau kuwa si kuomba kwenu. Lakini nyinyi mmemkadhibisha. Basi adhabu lazima iwe.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mwenyezi Mungu Anatoa habari kuwa Yeye hawajali watu wala hashughuliki nao lau si wao kumlingania Yeye ulinganizi wa ibada na ulinganizi wa maombi. Hakika yenu nyinyi, enyi makafiri, mumekanusha, na ukanushaji wenu utapelekea mupate adhabu yenye kuwa na nyinyi kama vile mwenye kudai anavyokuwa na mdaiwa wake, na Atawaangamiza duniani na Akhera.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس