وَبِكُفۡرِهِمۡ وَقَوۡلِهِمۡ عَلَىٰ مَرۡيَمَ بُهۡتَٰنًا عَظِيمٗا
Na pia kwa kufuru zao na kumsingizia kwao Maryamu uwongo mkubwa,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na vile vile tuliwalaani kwa sababu ya ukafiri wao na kumzulia kwao Maryam urongo kwa yale waliyomsingizia nayo ya uzinifu na hali yeye yupo mabali na hilo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس