وَإِن تُطِعۡ أَكۡثَرَ مَن فِي ٱلۡأَرۡضِ يُضِلُّوكَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ
Na ukiwat'ii wengi katika hawa waliomo duniani watakupoteza na Njia ya Mwenyezi Mungu. Hawa hawafuati ila dhana tu, na hawakuwa ila ni wenye kusema uwongo tu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau itakadiriwa, ewe Mtume, kwamba wewe uliwasikiliza wengi kati ya watu wanaokaa ardhini, kwa kweli wanagalikupoteza ukawa kando na dini ya Mwenyezi Mungu. Kwani wao hawaendi isipokuwa kwenye yale wanayoyaona kuwa ni haki kwa kuwaiga wakale wao. Na hawakuwa wao isipokuwa tu wanadhania na wanasema urongo.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس