وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَيۡنَ شُرَكَآؤُكُمُ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ
Siku tutapo wakusanya wote pamoja, kisha tuwaambie walio shirikisha: Wako wapi washirikishwa wenu mlio kuwa mnadai?
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na wajihadhari washirikina hawa wenye kuzikanusha aya za Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, na Siku ambayo tutawafufua kisha tutasema kuwaambia, «Wako wapi waungu wenu ambao mlikuwa mkidai kuwa wao ni washirika na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, ili wawaombee nyinyi?»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس