وَمَا تَأۡتِيهِم مِّنۡ ءَايَةٖ مِّنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِمۡ إِلَّا كَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ
Na haiwafikii hata ishara moja katika ishara za Mola wao Mlezi ila wao huwa wenye kuipa nyongo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Makafiri hawa Ambao wanamshirikisha mwingine na Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, wamejiwa na hoja zilizo wazi na dalili dhahiri juu upweke wa Mwenyezi Mungu, Aiyetukuka na kuwa juu, na ukweli wa Muhammad, rehema ya Mwenyezi Mungu na amani zimshukie, juu ya utume wake na yale aliyokuja nayo. Lakini punde tu yalipowajia waliyaepuka na kukataa kuyakubali na wasiyaamini.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس