۞وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ ءَازَرَ أَتَتَّخِذُ أَصۡنَامًا ءَالِهَةً إِنِّيٓ أَرَىٰكَ وَقَوۡمَكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake, Azar: Unayafanya masanamu kuwa ni miungu? Hakika mimi nakuona wewe na watu wako mmo katika opotofu ulio wazi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na kumbuka, ewe Mtume, mahujiano ya Ibrāhīm, amani imshukiye, na baba yake Āzar. Ibrāhīm alipomwambia, «Je, unawafanya masanamu ni waungu, unawaabudu badala ya Mwenyezi Mungu Aliyetukuka? Mimi nakuona wewe na watu wako muko kwenye upotevu uliyo wazi, muko kando na njia ya haki.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس