وَلِلَّهِ غَيۡبُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَإِلَيۡهِ يُرۡجَعُ ٱلۡأَمۡرُ كُلُّهُۥ فَٱعۡبُدۡهُ وَتَوَكَّلۡ عَلَيۡهِۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ
Na ni vya Mwenyezi Mungu tu vyote vilivyo fichikana katika ardhi na mbingu, na mambo yote yatarejezwa kwake. Basi muabudu Yeye na umtegemee Yeye. Na Mola wako Mlezi haghafiliki na yale mnayo yatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Ni wa Mwenyezi Mungu, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake na kutukuka ni Kwake, ujuzi wa kila kisichoonekana mbinguni na ardhini. Na Kwake yanarejeshwa mambo yote Siku ya Kiyama. Basi muabudu Yeye, ewe Nabii, na umtegemezee mambo yako Kwake. Na Mola wako Hakuwa ni mwenye kughafilika na yale mnayoyafanya ya wema na uovu na Atamlipa kila mtu kwa matendo yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس