إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَأَخۡبَتُوٓاْ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Hakika wale walio amini, na wakatenda mema, na wakanyenyekea kwa Mola wao Mlezi, hao ndio watu wa Peponi, na humo watadumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Hakika wale ambao walimuamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na wakafanya matendo mema, wakanyenyekea kwa Mwenyezi Mungu katika kila walichoamrishwa na kukatazwa. Hao ndio watu wa Peponi, hawatakufa humo wala hawatatoka kabisa.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس