وَلَا يَنفَعُكُمۡ نُصۡحِيٓ إِنۡ أَرَدتُّ أَنۡ أَنصَحَ لَكُمۡ إِن كَانَ ٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يُغۡوِيَكُمۡۚ هُوَ رَبُّكُمۡ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ
Wala nasaha yangu haikufaini kitu nikitaka kukunasihini, ikiwa Mwenyezi Mungu anataka kukuachieni mpotee. Yeye ndiye Mola wenu Mlezi; na kwake mtarejeshwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na hautawanufaisha nyinyi ushauri wangu na bidii yangu katika kuwalingania kwenye Imani, iwapo Mwenyezi Mungu Anataka kuwpoteza na kuwaangamiza. Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, Ndiye mwenye kuwamiliki, na Kwake Yeye mtarejeshwa kesho Akhera kwa kuhesabiwa na kulipwa.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس