فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ مَن يَأۡتِيهِ عَذَابٞ يُخۡزِيهِ وَيَحِلُّ عَلَيۡهِ عَذَابٞ مُّقِيمٌ
Nanyi mtakuja jua ni nani itakaye mfikia adhabu ya kumhizi, na itakaye mteremkia adhabu ya kudumu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Mtajua hapo, itakapokuja amri ya Mwenyezi mungu kwa hilo, ni yupi yule ambaye itamjia , hapa ulimwenguni, adhabu ya Mwenyezi Mungu yenye kumtweza na itamshukia, huko Akhera, adhabu ya daima isiyokatika.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس