وَيَٰقَوۡمِ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِ يُرۡسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡكُم مِّدۡرَارٗا وَيَزِدۡكُمۡ قُوَّةً إِلَىٰ قُوَّتِكُمۡ وَلَا تَتَوَلَّوۡاْ مُجۡرِمِينَ
Na enyi watu wangu! Muombeni msamaha Mola wenu Mlezi, kisha mtubie kwake. Atakuleteeni mbingu zenye kunyesha mvua ya kumiminika, na atakuzidishieni nguvu juu ya nguvu zenu. Wala msigeuke mkawa wakosefu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Enyi watu wangu, takeni msamaha wa Mwenyezi Mungu kwa kumuamini Yeye, kisha mtubie Kwake kutokana na dhambi zenu. Kwani nyinyi mkifanya hivyo, Atawateremshia mvua yenye kufuatana iliyo nyinygi, hivyo basi mazuri yenu yatakuwa mengi na Atawaongezea nguvu juu ya nguvu mlizonazo kwa wingi wa watoto wenu na mfuatano wa neema juu yenu. Na msiyape mgongo yale ninayowalingania nyinyi kwayo mkawa ni wenye kuendelea juu ya makosa yenu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس