وَٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِۚ إِنَّ رَبِّي رَحِيمٞ وَدُودٞ
Na ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi, tena tubuni kwake. Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kurehemu na Mwenye upendo.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na ombeni kutoka kwa Mola wenu msamaha wa dhambi zenu, kisha rudini kumtii na endeleeni juu yake. Hakika Mola wangu ni Mwingi wa rehema, ni Mwingi wa mapenzi na mahaba kwa aliyetubia na akarejea Kwake.» Katika hii aya, pana kuthibitisha sifa ya raḥmah (kurehemu) na mawaddah (kupenda) kwa Mwenyezi Mungu, Aliyetukuka, kama inavyonasibiana na Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس