قَالُواْ يَٰشُعَيۡبُ مَا نَفۡقَهُ كَثِيرٗا مِّمَّا تَقُولُ وَإِنَّا لَنَرَىٰكَ فِينَا ضَعِيفٗاۖ وَلَوۡلَا رَهۡطُكَ لَرَجَمۡنَٰكَۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡنَا بِعَزِيزٖ
Wakasema: Ewe Shua'ibu! Mengi katika hayo unayo yasema hatuyafahamu. Na sisi tunakuona huna nguvu kwetu. Lau kuwa si jamaa zako tunge kupiga mawe, wala wewe si mtukufu kwetu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Walisema, «Ewe Shu'ayb! Hatuyafahamu mengi unayotwambia, na sisi tunakuona wewe kuwa ni mnyonge kwetu, wewe si miongoni mwa watu wakubwa wala viongozi, na lau sisi si kuwastahi jamaa zako tungalikuua kwa kukupiga mawe.»- Na kundi la jamaa zake lilikuwa ni katika watu wanaofuata mila yao.- «Na wewe huna cheo wala heshima katika nafsi zetu.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس