قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَهۡطِيٓ أَعَزُّ عَلَيۡكُم مِّنَ ٱللَّهِ وَٱتَّخَذۡتُمُوهُ وَرَآءَكُمۡ ظِهۡرِيًّاۖ إِنَّ رَبِّي بِمَا تَعۡمَلُونَ مُحِيطٞ
Akasema: Enyi watu wangu! Kwani jamaa zangu ni watukufu zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu? Na Yeye mmemueka nyuma ya migongo yenu! Hakika Mola wangu Mlezi ni Mwenye kuyazunguka yote mnayo yatenda.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Akasema, «Enyi watu wangu! Kwani jamaa zangu ni wenye nguvu zaidi na ni watukufu zaidi kwenu kuliko Mwenyezi Mungu? Na mumeitupa amri ya Mola wenu, mkaiweka nyuma ya migongo yenu, mkawa hamjilazimishi kufuata amri Zake na hamjiepushi na makatazo Yake. Hakika Mola wangu ni kwa mnayoyafanya Ameyazunguka, hakuna chochote katika matendo yenu kinafichika Kwake hata kama kina uzito wa chungu mdogo, na Atawalipa kwa hizo kwa haraka au baadaye.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس