وَيَٰقَوۡمِ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنِّي عَٰمِلٞۖ سَوۡفَ تَعۡلَمُونَ مَن يَأۡتِيهِ عَذَابٞ يُخۡزِيهِ وَمَنۡ هُوَ كَٰذِبٞۖ وَٱرۡتَقِبُوٓاْ إِنِّي مَعَكُمۡ رَقِيبٞ
Na enyi watu wangu! Fanyeni mwezayo, na mimi pia ninafanya. Karibuni mtajua ni nani itakaye mfikia adhabu ya kumhizi, na nani aliye mwongo. Na ngojeni, mimi pia ninangoja pamoja nanyi.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
«Na enyi watu wangu! Fanyeni mnaloliweza kwa njia yenu na namna yenu. Mimi ni mwenye kuendelea kufanya kwa njia yangu na nikitumia kile Mwenyezi Mungu Amenipa cha kuwalingania nyinyi kwenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu. Mtajua ni nani miongoni mwetu, itamjia adhabu yenye kumfanya mnyonge, na ni nani, miongoni mwetu, ni mrongo katika maneno yake: ni mimi au ni nyinyi? Na mngojee kitakachowashukia; mimi ni miongoni mwa wenye kungojea pamoja na nyinyi.» Hili ni onyo kali kwao.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس