وَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلۡقُرۡءَانُ جُمۡلَةٗ وَٰحِدَةٗۚ كَذَٰلِكَ لِنُثَبِّتَ بِهِۦ فُؤَادَكَۖ وَرَتَّلۡنَٰهُ تَرۡتِيلٗا
Na wakasema walio kufuru: Kwa nini hakuteremshiwa Qur'ani kwa jumla moja? Hayo ni hivyo ili tuuthibitishe moyo wako, na ndio tumeisoma kwa mafungu.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na Waliokanusha walisema, «Si hii Qur’ani ateremshiwe Muhammad kwa mara moja» kama ilivyokuwa Taurati, Injili na Zaburi? Mwenyezi Mungu, Aliyetakasika na kutukuka, Akasema «Tumeiteremsha ikiwa hivyo, sehemu-sehemu, ili kuutia nguvu moyo wako na ili wewe uzidi utulivu, upate kuielewa na kuibeba, na tumeifunua wazi kwa kuithibitisha na kwa kuileta polepole.»
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس