ٱنظُرۡ كَيۡفَ ضَرَبُواْ لَكَ ٱلۡأَمۡثَٰلَ فَضَلُّواْ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ سَبِيلٗا
Tazama jinsi wanavyo kupigia mifano. Basi wamepotea, wala hawataiweza Njia.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Tazama, ewe Mtume, namna walivyosema, hawa wakanushaji, juu yako maneno hayo ya ajabu yanayofanana na mifano kwa ugeni wake, ili wafikie kukukanusha, kwa hivyo wakawa mbali na haki, na kwa hivyo hawapati njia ya kuifikia (hiyo haki) ili wayarakibishe maneno waliyoyasema kuhusu wewe, ya urongo na uzushi.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس