ذَٰلِكَ ٱلۡفَضۡلُ مِنَ ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ عَلِيمٗا
Hiyo ni fadhila itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mjuzi wa kutosha.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Vipewa vingi hivyo vinatoka kwa Mwenyezi Mungu Peke Yake. Na inatosha kuwa Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Anazijua hali za waja Wake na Anawajua wenye kustahiki thawabu nyingi kati yao kwa matendo mema waliyoyafanya.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس