وَلَا تَرۡكَنُوٓاْ إِلَى ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ فَتَمَسَّكُمُ ٱلنَّارُ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِنۡ أَوۡلِيَآءَ ثُمَّ لَا تُنصَرُونَ
Wala msiwategemee wanao dhulumu, usije ukakuguseni Moto. Wala nyinyi hamna walinzi badala ya Mwenyezi Mungu, wala tena hamtasaidiwa.
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Wala msilemee upande wa hawa makafiri walio madhalimu, msije mkapatwa na Moto. Na hamna nyinyi msaidizi mwenye kuwanusuru na kusimamia mambo yenu isipokuwa Mwenyezi Mungu.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس