وَلَوۡ شَآءَ رَبُّكَ لَجَعَلَ ٱلنَّاسَ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗۖ وَلَا يَزَالُونَ مُخۡتَلِفِينَ
Na Mola wako Mlezi angeli penda ange wafanya watu wote wakawa umma mmoja. Lakini hawaachi kukhitalifiana,
Ali Muhsin Al - Swahili translation
Na lau Mola wako Alitaka, Angaliwafanya watu wote ni kundi moja, wako kwenye dini moja , nayo ni dini ya Uislamu. Lakini Yeye, kutakata na sifa za upungufu ni Kwake, hakutaka hivyo. Basi watu hawataacha kuendelea kutafautiana katika dini zao, na hayo ndiyo yanayoambatana na hekima Yake.
الترجمة السواحلية - عبد الله محمد وناصر خميس